Hii ni baada ya mchezaji huyo
kupata jeraha kwenye misuli ya paja. Mchezaji huyo wa kimataifa wa Ufaransa
aliumia kipindi cha pili cha mechi ya ligi ndogo ya klabu Ulaya, Europa League,
kati ya United na FC Rostov ya Urusi na ikamlazimu kuondoka uwanjani ambapo nafasi
yake ilijazwa na Marouane Fellaini.
Manchester United walishinda 1-0 kupitia bado la Juan Mata na
wakasonga hati robofainali kwa ushindi wa jumla wa 2-1 dhidi ya Rostov.
Pogba mwenye umri wa miaka 24,
pia anatarajiwa kukosa pia mechi za timu ya taifa ya Ufaransa dhidi ya
Luxembourg na Uhispania baadaye mwezi huu hata hivyo meneja wa United Jose
Mourinho hakusema Pogba anatarajiwa kukaa nje muda gani.
Alipoulizwa iwapo huenda ikawa karibu wiki tatu, Mourinho alisema:
"Kweli. Lakini sina uhakika, lakini kwa kweli hawezi kucheza dhidi ya
Middlesbrough na hatachezea timu ya taifa."
Pogba ndiye mchezaji
aliyenunuliwa ghali zaidi duniani na amefungia timu hiyo mabao saba na kusaidia
ufungaji wa mengine matano katika mechi 41 alizowachezea msimu huu.
0 comments:
Post a Comment