Rais wa jamhuri ya muungano wa Tanzana Dkt. John Pombe Magufuli
amefuta agizo lililotolewa na Waziri Wa Katiba na Sheria, Dkt. Haryson
Mwakyembe lenye sharti la kuwa na cheti cha kuzaliwa Kwa yeyote atakayehitaji
kufunga ndoa kuanzia tarehe 1 Mei mwaka huu.
Taarifa hiyo imetolewa leo mara baada ya agizo hilo kutolewa jana
na waziri Mwakyembe, lengo ikiwa ni kutaka kuzuia wahamiai haramu na kuwepo kwa
taarifa muhimu za watu zitakazosaidia kuweka mipango ya maendeleo endelevu.
Rais Magufuli ametoa taarifa hiyo ya kufuta agizo hilo alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari mjini Dodoma kbala ya kuondoka Ikulu ya Chamwino
0 comments:
Post a Comment