SHIRIKA LA AFYA DUNIANI, WHO KUISAIDI AFRIKA KUPAMBANA NA UGONJWA WA KUPOOZA

Shirika la Afya Duniani limesema watoto milioni 116 watapa chanjo ya ugonjwa wa kupooza wa polio katika nchi 13 za Afrika magharibi na Afrika ya Kati kama sehemu ya jitihada za kuangamiza maradhi hayo barani Afrika.
Mpango huo utawalenga watoto wote wa chini ya miaka mitano katika nchi hizo 13 ikiwamo Benin, Cameroon, Jamhuri ya Afrika ya Kati, Chad, Côte d'Ivoire, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Guinea, Liberia, Mali, Mauritania, Niger, Nigeria na Sierra Leone.

Mkurugenzi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linalowahudumia watoto UNICEF kwa nchi za Afrika magharibi na Afrika ya Kati Marie-Pierre Poirier amesema ana matumaini kuwa ugonjwa wa polio utatokomewzwa barani humo kwa msaada wa viongozi wa Kiafrika
Share on Google Plus

About Unknown

0 comments:

Post a Comment