TANESCO YADAIWA ZAIDI YA BILIONI (4) NNE


Shirika la umeme Tanzania (Tanesco), linadaiwa zaidi ya shilingi bilioni 4 na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) za kodi ya mitambo ya kuzalisha umeme iliyokwama katika Mamlaka ya Bandari Tanzania.
Akizungumza na wanahabari Kaimu Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini, Deo Ngalawa, baada ya kutembelea mradi wa uzalishaji wa umeme wa gesi asilia wa Kinyerezi, Dar es Salaam, alisema kuwa mitambo hiyo iliingizwa nchini ili kuongeza uzalishaji wa umeme.
“Tanesco inadaiwa zaidi ya shilingi bilioni 4 na TRA, deni hilo linatokana na kukwama kwa mizigo ya kuzalisha umeme, ikiwamo mitambo na jenereta kutoka nje ya nchi, jambo ambalo linachangia kurudisha nyuma uzalishaji wa umeme,” alisema Ngalawa.
Aidha alisema maeneo mengi ya mradi huo yanahitaji kuwekwa mitambo ambayo imezuiliwa kutoka kutokana na deni hilo, hivyo watazungumza na serikali kuona namna ya kutatua changamoto hiyo.


Share on Google Plus

About Unknown

0 comments:

Post a Comment