Kamanda wa polisi
kanda Maalum ya Dar es Salaam, Simon Sirro amesema kuwa kuna baadhi ya wasanii
ambao hawapokei simu wakidhani wakipigiwa itakuwa ni suala la dawa za kulevya.
Kamanda Sirro
ameyasema hayo Jumatano ya tarehe 15 mwezi Machi katika maadimisho ya mwaka
mmoja ya ukuu wa mkoa, ambapo maadh7=imisho hayo yalikuwa maalum kwa ajili ya
mkuu wa mkoa wa Dar es salaam amabaye ametimiza mwaka mmoa tangu kuteuliwa
kwake na Rais wa Jamuhuri ya Muungano ya Tanzania Dkt John Pombe Magufuli.
“Awali ya yote Kwanza nimpongeze Mkuu wa Mkoa
wa Dar es salaam, Paul Makonda kwa kutimiza mwaka mmoja lakini pia nimpongeze
kwa kuwaleta vijana wetu hasa wale waliokuwa wanatumia madawa ya kulevya.
Kwangu ni siku ya furaha kwasababu tangu hili zoezi lianze hata nikiwapigia
simu wasanii kama wakina Banana Zoro hawapokei simu, hata viongozi wa dini
hivyo hivyo lakini hii inaonesha kwamba kila mtu anajua umuhimu wa suala hili”
Alisema Kamanda Sirro.
0 comments:
Post a Comment