Wachezaji wa timu ya taifa ya Uingereza Wayne Rooney na Harry
Kane wamepata mrithi atakayeziba pengo la uwepo wao kutokana na maeruhi
waliyoyapata. Rooney na Kane walitarajiwa kuwa katika kikosi cha timu ya
Uingereza kitakachovaana na timu ya taifa ya Ujerumani katika mechi ya kirafiki
kabla ya mchuano wa Kombe la Dunia dhidi ya Lithuania huko
Wembley tarehe 26 mwezi Machi.
Rashford
ambaye mechi yake ya kwanza kuichezea Uingereza alifunga goli walipopata
ushindi wa magoli 2-1 dhidi ya Australia mwezi Mei mwaka Jana na wamejizolea
vikombe sita vikuu.
Manchester United ilimchezesha waliposhindwa kwa bao 1-0 dhidi
ya Chelsea katika kombe la FA siku ya Jumatatu , licha ya kutolewa katika
kikosi cha hapo awali kutokana na maradhi.Nahodha wa Uingereza, Rooney alikuwa
nje wakati Manchester United ilipo kutana na Chelsea kutokana na jeraha
alilolipata alipogongana na mwenzake walipokuwa wakifanya mazoezi.
Na
mshambuliaji wa Tottenham, Harry Kane pia alitolewa nje ya uwanja kutokana na
jeraha la kifundo cha mguu walipokuwa wakicheza na Millwall siku ya Jumapili. Klabu
ya Spurs imesema jeraha hilo linafanana na lile alilolipata mwezi Septemba
wakikabiliana na Sunderland
0 comments:
Post a Comment