Waziri wa Nishati, Prof. Muhongo amewatoa hofu wananchi wa
Zanzibar kuwa hawatakatiwa umeme baada ya SMZ kuanza kulipa deni inalodaiwa ni
baada ya siku chache tangu itangazwe kwamba Zanzibar itazimiwa umeme endapo
haitalipa deni hilo.
Tayari
Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar imeanza kulipa deni la shilingi bilioni 10
linalodaiwa na shirika la umeme Tanzania TANESCO, na itaendele kulipa deni hilo
mpaka litakapomalizika.
“Tayari Serikali
ya Mapinduzi ya Zanzibar imeanza kulipa
kiasi cha Shilingi bilioni 10 na itaendelea kulipa deni hilo mpaka litakapomalizika”
alisema Prof. Muhongo.
0 comments:
Post a Comment