MADAKTARI WALIOTAKIWA KWENDA KENYA WAITWA KAZINI RASMI


Madaktari waliotakiwa kwenda kuhudumu nchini Kenya kulikokuwa na uhaba wa madaktari kutokana na mgomo wa madaktari nchini humo wameitwa kazini rasmi na wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto. Tangazo hilo limekuja mara moja kufuatia agizo la Rais la kuwapatia kazi madaktari hao walioonesha nia ya kwenda kufanya kazi nchini Kenya.
Tangazo hilo limetolewa na katibu wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto na kuwataka madaktari hao kuripoti kwenye vituo vyao vya kazi siku kumi nan ne (14) kuanzia siku ya tangazo hili. Waliopamgiwa TAMISEMI wametakiwa kuripoti Ofisi za TAMISEMI Ddodoma na waliopangiwa wizarani warripoti Ofisi ndogo za Wizara Dar es Salaam

Share on Google Plus

About Unknown

0 comments:

Post a Comment