Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Ndug Martin Shighela, amesema Vita ya
madawa ya kulevya inaendelea hivyo kuviagiza vikosi vya Ulinzi na Usalama
kuhakikisha inawakamata vinara wa wasafirishaji na wauzaji.
Mkuu wa mkoa Martin Shighela akizungumza wakati wa hafla
hiyo
|
Akizungumza
katika hafla ya fupi ya makabidhiano ya jengo la Afya ya Akili Hospitali ya
Rufaa ya Bombo lililokarabatiwa na Kituo cha Tanga International Comperence
Centre (TICC), Shighela alisema vita ya madawa itakuwa endelevu.
Alisema vijana wengi wamekuwa wakiathirika na
matumizi ya madawa ya kulevya na Taifa kukosa nguvu kazi ya kuleta maendeleo na
kuviagiza vyombo vya ulinzi na usalama kuhakikisha Tanga hakuna njia ya
upitishaji.
“Kuna wagonjwa wa akili kutokana na maumbile yao lakini kuna
wagonjwa wengine wa akili wa kujitakia ambao sababu zake ni matumizi ya madawa
ya kulevya” alisema Shighela na kuongeza “Ili kuwaokoa vijana wetu na kupunguza
nguvu kazi naviagiza vyombo vya ulinzi na usalama kuongeza nguvu ya mapambano
ya madawa ya kulevya” alisema
Kwa upande wake Balozi wa Norway hapa nchini, Hanne-Marie
Karstand, amewataka watumishi wa hospitali ya Bombo kulitunza jengo hilo kama
ilivyo matumizi yake.
Alisema Serikali ya Norway itaisaidia Tanzania katika Nyanja
mbalimbali za kijamii ikiwemo Afya, elimu, Mazingira pamoja na wagonjwa wa Afya
ya Akili.
Balozi wa Norway hapa
nchini Hanne-Marie
|
0 comments:
Post a Comment