WATUHUMIWA WENGINE WATATU WA MAUAJI YA POLISI NANE KIBITI WAUAWA


Watu watatu wanaodaiwa kuwa miongoni mwa waliohusika kuwaua viongozi wa vijiji na askari polisi nane katika wilaya za Mkuranga, Kibiti na Rufiji mkoani Pwani wameuawa na jeshi la polisi mkoani humo kwa kupigwa risasi.

Kamanda wa jeshi la polisi mkoani Pwani Onesmo Lyanga amedai kuwa watu hao wamefariki dunia walipokuwa wakipelekwa hospitali ya Mission ya Mchukwi kwa matibabu baada ya kujehiwa na risasi miguuni na kiunoni.

Askari polisi waliamua kuchukua uamuzi huo baada ya watu hao kukaidi amri halali ya polisi ya kuwataka wasimame baada ya kuwatilia mashaka na kukimbilia porini wakiwa kwenye pikipiki, watu hao walikuwa katika pikipiki tatu hukumbili kati ya hizo zilikuwa zimewabeba watu waliovalia hijabu wakitokea Kibiti katika barabara kuu ya Dar-Lindi.

Kamanda Laynga ameeleza kwamba askari wa kituo cha Mwembe Muhoro waliwasimamisha watu lakini walikaidi amri hiyo, ndipo askari walipochukua hatua ya kuwafuatilia huku wakifyatua juu risasi kuwaonya kabla ya watu hao kuruka kutoka kwenye pikipiki na kukimbilia maporini, kitendo kilichowafanya askari kuwafyetulia risasi watu hao.


Kamanda pia ameongeza kuwa watu hao waliokuwa wamevalia hijabu walitambulika kuwa walikuwa wanaume waliotumia pikipiki aina ya Boxer yenye namba MC 272 BLW za usajili.  
Share on Google Plus

About Unknown

0 comments:

Post a Comment