CHAMA CHA MAPINDUZI KUWASAIDIA WALIOKOSA MIKOPO YA ELIMU YA JUU

Chama cha Mapinduzi (CCM) kimewaita wanafunzi wote wa elimu ya juu nchini ambao wamekosa mikopo ya elimu yajuu kutokana na sababu mbalimbali, chama hiko kimewataka wanafunzi hao kufika katika ofisi ndogo za chama hicho zilizopo mtaa wa Lumumba jijini Dar es Salaam.                             Katika taarifa iliyochapishwa kwenye ukurasa wa Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Humphrey Polepole iliwataka wanafunzi wote ambao ni yatima, wenye ulemavu na ambao wazazi wao ni walemavu lakini wamekosa mkopo wamefika katika ofisi za CCM.
Taarifa hiyo iliyotolewa Julai 20 mwaka huu haikufafanua zaidi ni hatua gani zitakazochukuliwa ili kuweza kuwasaidia wanafunzi hao walioitwa.

Akizungumzia hatua hiyo, Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu Tanzania (TAHLISO), Stanslaus Kadugazile alisema hilo ni jambo jema na kwamba ni la kupongezwa zaidi kwa kuwa wamewaita wote bila kuwabagua kivyama.
Share on Google Plus

About Unknown

0 comments:

Post a Comment