MAREKANI KUPIGA MARUFUKU SAFARI ZA KOREA KASKAZINI

Nchi ya Marekani kupiga marufuku raia wake kusafiri kwenda nchini Korea Kaskazini, kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na mashirika mawili yanayofanya kazi ya kupanga safari za kwenda nchini Korea Kaskazini japo Seriakli ya Marekani bado haijathibitisha taarifa hizo.
Mashirika hayo ya Koryo Tours na Young Pioneer Tours yamesema marufuku hiyo itatangazwa tarehe 27 Julai na itaanza kutekelezwa siku 30 baadaye. Shirika la Young Pioneer Tours ndilo lililofanikisha mwanafunzi Mmarekani Otto Warmbier kuzuru Korea Kaskazini ambaye likamatwa baadaye muda mfupi kabla yake kuondoka nchini humo na kuhukumiwa kufungwa jela miaka 15.
Hata hivyo, alirejeshwa Marekani mwezi Juni akiwa amepoteza fahamu na akafariki dunia wiki moja baadaye.
Shirika hilo, lenye makao yake China, imesema haitasaidia Wamarekani wengine kuingia Korea Kaskazini. Shirika hilo lilitoa taarifa Ijumaa na kusema: "Tumefahamishwa sasa hivi kwamba serikali ya Marekani haitawaruhusu tena raia wa Marekani kusafiri DPRK (Korea Kaskazini).
"Inatarajiwa kwamba marufuku hiyo itaanza kutekelezwa katika kipindi cha siku 30 kuanzia Julai 27. Baada ya kipindi hicho cha siku 30 raia yeyote wa Marekani ambaye atasafiri Korea Kaskazini atafutiwa pasipoti yake na serikali ya taifa lake."
Rowan Beard, wa Young Pioneer Tours, wameliambia shirika la utangazaji la Uingereza BBC kuwa shirika hilo limefahamishwa hayo na ubalozi wa Sweden, ambao hushughulikia masuala ya Marekani nchini Korea Kaskazini, pia ubalozi huo unajaribu kujua idadi ya watalii kutoka Marekani ambao bado hawajaondoka Korea Kaskazini.
Bw Beard amesema ubalozi huo unawahimiza raia wa Marekani kuondoka nchini humo mara moja, amesema nafuu hiyo ya siku 30 "itawapa fursa (Wamarekani) wowote ambao kwa sasa wamo nchini humo kama watalii ama wakifanya kazi za kibinadamu."
Naye Simon Cockerill, wa Koryo Tours, ameliambia Shirika la Utangazaji la Uingereza BBC kuwa amepashwa habari na ubalozi wa Sweden, amesema shirika hilo bado litaendelea kupanga safari na kupeleka Wamarekani Korea Kaskazini hadi marufuku hiyo ianze kutekelezwa.
"Ni habari za kusikitisha sana kwa sekta hii na pia kwa raia wa Korea Kaskazini ambao wanataka kuwafahamu zaidi Wamarekani|” amesema Bw Cockerill


Share on Google Plus

About Unknown

0 comments:

Post a Comment