NKURUNZINZA AMEFANYA ZIARA TANZANIA NA KUWATAKA WARUNDI WARUDI NCHINI KWAO

Rais wa Jamhuri ya Burundi Mhe. Piere Nkurunzinza leo tarehe 20 Julai, 2017 amefanya ziara ya rasmi ya kiserikali ya siku moja hapa nchini kwa mwaliko wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Johnh Pombe Magufuli.
Ziara hiyo imefanyika katika wilaya ya Ngara mkoani Kagera ambapo Mhe. Raios Nkurunzinza amepokelewa rasmi kwa kupigiwa mizinga 21 na kukagua gwaride rasmi lililoandaliwa na Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) kwa heshima yake katika eneo la Lemela na baadaye mazungumzo rasmi na dhifa ya kitaifa iliyofanyika Ngara.

Akizungumza katika mkutano huo Rais Magufuli aliyeongozana na mkewe Mama Janeth Magufuli amemshukuru Mhe. Rais Nkurunzinza kwa kukubali mwaliko wake na amehakikisha kuwa serikali yake ya awamu ya tano itaendeleza na kuimarisha uhusiano na ushirikiano wa kihistoria na kindugu nan chi ya Burundi hususani katika kukuza Biashara na Uwekezaji.
“Tanzania ni ndugu zako na watanzania ni ndugu wa watu wa Burundi, umekuja kwa mazungumzo ya kiuchumi, tumezungumza mambo mengi ya kuimarisha biashara kati ya Tanzania na Burundi, katika takwimu za mwaka 2016 biashara kati ya Tanzania na Burundi ilikuwa na thamani ya Shilingi Milioni 116.5, kiwango hiki ni kidogo kwa nchi ya Burundi ambayo ina watu Zaidi ya Milioni 10 na Tanzania ambayo ina watu Zaidi ya Milioni 52” amesema Mhe. Rais Magufuli
Mbali na hayo Rais Magufuli aliligusia suala la hali ya wakimbizi kutoka Burundi ambao walikimbilia nchini Tanzania kipindi cha machafuko ya kisiasa. Rais Magufuli amesema kuwa wakjimbizi waliokimbilia kutoka nchini Burundi ni wakati sasa kurudi nyumbani kwani jitihada za Mhe. Rais Nkurunzinza za kulinda Amani zimeleta matunda.
Aidha Rais Magufuli amemuagiza Waziri wa Mambo ya Ndani Mhe. Mwigulu Nchemba kusitisha utoaji wa uraia kwa wakimbizi hao ili utaratibu huo usitumike kama kigezo cha wao kuzikimbia nchi zao.
Naye Mhe. Rais Nkurunzinza amemshukuru Rais Magufuli kwa mwaliko na kutoa Wito kwa wafanyabiashara wa Burundi na wafanyabiashara wa Tanzania kushirikiana katika biashara pia amesema kuwa hali ya Burudni ni shwari kwani hata wakimbizi walioikimbia Burundi na kukimbilia Tanzania miaka miwili iliyopita wanaendelea kurudi nchini Burundi na kuendelea na shughuli zao za kimaendeleo.

“Nataka kuwajulisha wenzetu watanzania na waurndi wenzetu ambao walikimbilia Tanzania, Burundi la leo ni nchi yenye Amani, tunawaalika Warundi wenzetu, kaka zetu, na dada zetu waliokimbilia hapa Tanzania, warudi nchini kwao tujenge nchi yetu iwe na Amani ya kudumu” amesema Rais. Nkurunzinza
Share on Google Plus

About Unknown

0 comments:

Post a Comment