TLS YALAANI KUKAMATWA KWA RAIS WAKE MHE. TUNDU LISSU

Baraza la Uongozi la Chama Cha Mawakili wa Tanganyika (Tanganyika Law Society TLS) kimesema kuwa kimelaani kitendo cha jeshi la polisi kumkamata na kuendelea kumshikilia Rais wa Chama hiko cha Mawakili Mhe. Tundu Antipus Lissu jana jioni akiwa uwanja wa ndege wa kimataifa wa Julius Nyerere alipokuwa akijiandaa kuelekea nchini Rwanda kuiwakiloisha TLS kwenye kikao cha Braza la Chama cha Mawakiliwa Africa Mashariki ambacho kinafanyika leo.

Mhe. Tundu Lissu anashikiliwa na Polisi kwa makosa ya uchochezi ambayo tayari alionywa na serikali kuacha kuendelea kutoa kauli za uchochezi na kupotosha umma.

Chama hiko Cha Wanasheria kimetoa wito kwa Jeshi la Polisi kumpatia Dhamana Mhe. Tundu Lissu pamoja na kumfikisha mahakamani ndani ya muwa wa kisheria kama ambavyo sharia za nchi zinavyoelekeza. 
Share on Google Plus

About Unknown

0 comments:

Post a Comment