Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Mhe.
Ally Hapi leo amefanya mkutano wa hadhara na wananchi wa maeneo ya Nakasangwe,
Nakalekwa na kumaliza mgogoro wa ardhi uliodumu eneo hilo kwa miaka 13 na
kusababisha vifo.
DC Ally Hapi |
Hapi amesema kuwa ikiwa ni
muendelezo wa utatuzi wa migogoro ya ardhi wilayani Kinondoni ofisi yake ilizikutanisha pande mbili za
wenye mashamba na wakazi ambazo kwa miaka kadhaa zimekua kwenye mgogoro mkubwa
na kufanya nao mazungumzo yaliyoweka msingi mzuri wa kumaliza mgogoro huo.
DC Hapi aliwaambia wakazi wa
maeneo hayo kuwa upimaji wa viwanja utafanyika na wote waliohakikiwa watapewa
viwanja vyao
"Tumeamua sasa eneo hili
lote lipimwe viwanja, ili wakazi wote mliohakikiwa kila mmoja apate kipande cha
ardhi cha kuishi na familia yake na viwanja vinavyobaki wapate wenye mashamba.
Hii ndiyo njia pekee ya kuweza kuwafanya muishi kwa amani katika mji uliopimwa
na kupangwa vizuri." Alisema DC Hapi
Aidha, Hapi aliwaeleza
wananchi hao kuwa katika eneo hilo zaidi ya viwanja 6000 vitapatikana na hivyo
kuwatoa shaka kuwa wakazi wote zaidi ya 3000 waliohakikiwa kila mmoja atapata
ardhi iliyopimwa huku wenye mashamba nao wakipata viwanja vitakavyobakia ili
waweze kuviendeleza au kuviuza vikiwa na hati miliki.
DC Hapi amesema kazi ya
upimaji wa ardhi katika eneo hilo inatarajiwa kuanza haraka na kumalizika ndani
ya kipindi cha miezi mitatu chini ya kampuni ya Afro Map ambayo pande mbili
zimeichagua kufanye kazi hiyo.
"Nawapa kampuni hii miezi
mitatu tu, kazi ya upimaji iwe imekamilika eneo hili ili wananchi wangu waishi
kwa amani wakijua serikali yao ipo kuwasaidia." Alisema DC.
Mgogoro wa Nakasangwe ulianza
mwaka 2004 na hivyo kudumu kwa miaka 13 kipindi ambacho kilitawaliwa na chuki,
uhasama na uadui mkubwa baina ya wenye mashamba na wananchi waliovamia mashamba
hayo. Watu kadhaa walipoteza maisha katika mgogoro huo.
Wananch wote wanaounda pande
mbili za mgogoro wamemshukuru DC Hapi na kushikana mikono kama ishara ya mwisho
wa mgogoro huo na mwanzo mpya.
0 comments:
Post a Comment